Thursday, May 30, 2013

SYRIA YAPATA ZANA MPYA ZA MPYA ZA KIVITA KUTOKEA URUSI

Syria imepokea zana za kisasa za kivita kutokea Urusi. Zana hizo zijulikanazo kwa jina la S-300 zina uwezo wa kuzuia makombora ya angani na ya ardhini. Maelezo hayo yametolewa na Rais Bashar Al-Assad. Rais huyo amedai kuwa ndo kwanza pamekucha na vita bado Mbichi na ndo inaanza kushika kasi. Aliyasema hayo kupitia kituo cha televisheni chenye mahusiano ya kikundi cha Hizbollah. Urusi imeahidi kuendelea kuihami Syria baada ya nchi hiyo kuondolewa vikwazo vya silaha. Wachambuzi wa mambo wanadai huenda nchi zinazojihusisha na mgogoro huu zikaanza kutumia silaha zake hasa baada ya Syria kusema kuwa ipo tayari kujibu mashambulizi yoyote na kulipiza kisasi dhidi ya Israel.Nae waziri wa mambo ya ndani wa Syria amesema sasa jeshi la Syria limerudi katika hali bora ya kupambana na waasi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO