Friday, June 28, 2013

EQUADOR YAAHIDI KUMPA UHURU SNOWDEN

Serikali ya Ecuador imempa pasi ya kusafiria afisaa wa zamani wa CIA Edward Snowden anaye tafutwa na serikali ya Marekani ambaye amekwama katika eneo la uwanja wa ndege wa Moscou ikiwa ni siku ya tano kwenye uwanja wa ndege wa Cheremetievo jijini Moscou akitokea Hong Kong Jumapili juma lililopita. Serikali ya Marekani ili sitisha kibali cha usafiri cha afisaa huyo wa zamani wa idara ya ujasusi nchini humo CIA na kudai kurejeshwa nyumbani kwa ajili ya kukabiliana na vyombo vya sheria kwa kosa la kuvujisha siri za taifa hilo kwenye nyanja ya ki elektroniki ambapi alisema Marekani imekuwa ikifanya uchunguzi wa mawasiliano ya ki elektroniki. Jambo ambalo lilizua tafrani kubwa.
Ubalozi mdogo wa Ecuador jijini London umetowa kibali cha usafiri kwa afisaa huyo wa zamani kitacho mrahisishia safari yake kuelekea nchini Ecuador ambako aliomba hifadhi ya kisiasa. Ubalozi huyo mdogo jijini London umezitaka nchi husika kumrahisishia afaisaa huyo na safari yake kuelekea katika nchi aliyo omba hifadhi. Kibali hicho chenye ukurasa mmoja chenye nembo ya Ecuador kimeaandika jina la Snwden, tarehe na mahali alipo zaliwa, rangi ya nywele zake na macho yake, urefu na hali ya familia na kutiwa sahihi na Fidel Narvaez Narvaez balozi mdogo wa Ecuador jijini London.
Hapo jana Ecuador ilikanisha taarifa za kutowa kibali cha usafiri kwa Edward Snowden afisaa wa samani wa idra ya ujasusi ya Marekani na kuweka ngumu kwenye ombi la ofisa huyo la kuomba hifadhi, na kutaja kuwa swala lake linaweza kuchukuwa siku au myezi. Ubalozi wa Ecuador jijini London ulimpa hifadhi pia Julian Assange, muasisi wa mtandao wa Wikileaks uliochapisha taarifa za siri mwaka 2010, kumlinda asisafirishwe kuelekea nchini Sweden ambako anakabiliwa na mashtaka ya ubakaji.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO