Friday, June 28, 2013

MORSI AONYA DHIDI YA MAANDAMANO

Rais wa Misri Mohammed Morsi ameonya kuwa vurugu za siasa zinaathiri demokrasia nchini humo. Katika hotuba ya taifa kupitia televisheni kuadhimisha mwaka mmoja tangu achukue uongozi, Bw Morsi alikiri kuwa amefanya makosa kadhaa. Kadhalika aliutaka upinzani kuwasilisha matakwa yake kupitia kura. Hata hivyo uongozi wake umekumbwa na changamoto si haba ambapo Misri imeshuhudia maandamano ya kila mara kati ya wafuasi na wapinzani wa Morsi.
Morsi pia amewonya wale wanaonekana kama wenye njama ya kutaabisha utawala wake na kujairbu kumwendea kichinichini pamoja na kusumbua demokrasia nchini humo. Wanajeshi wamepelekwa katika miji mikubwa kote nchini kabla ya kufanyika kwa maandamano yanayopangwa dhidi ya utawala wake mwishoni mwa wiki hii. Hotuba ya bwana Morsi imetolewa wakati makabiliano yakitokea Kaskazini mwa mji wa Mansoura.
Watu wawili waliuawa na wengine 170 kujeruhiwa kwenye mapigano kati ya wafuasi na wapinzani wa serikali, kwa mujibu wa afisaa wa afya. Morsi anayeongoza chama tawala cha Muslim Brotherhood, alikuwa rais wa kwanza wa taifa hilo kwa chama cha kiisilamu babada ya kushinda uchaguzi mwezi Juni mwaka jana. Uchaguzi huo ulisifiwa na wengi kuwa huru na wa haki. Mwaka wake wa kwanza mamlakani umekumbwa na maandamano ambayo hayaishi pamoja na uchumi unaodorora.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO