Friday, June 28, 2013

ZUMA AFUTA ZIARA ZAKE KUFATIA KUUMWA KWA MANDELA

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amefuta safari yake katika nchi za nje ili kubaki nchini mwake wakati huu kinara wa ubaguzi wa rangi Nelson Mandela akiwa katika hali mahtuti jijini Pretoria, ambapo ametowa wito kwa wananchi kuendelea kumuombea. Hii ni mara ya kwanza rais wa taifa hilo anapangua ratiba tangu kulazwa hospitalini kwa kinara mtetezi wa ubaguzi wa rangi. Usiku mzima watu walijitokeza kwa wingi na mishumaa katika Hospitali ya Mediclinic Heart Hospital ambako amelazwa kinara huyo, ishara ya upendo dhidi ya kinara huyo.
Mandela ambaye tangu siku ya Jumapili hali yake imekuwa mbaya mno, kwa sasa anapumua kwa nguvu za machine, ambapo kiongozi wa jadi wa ukoo wa Mandela, Napilisi Mandela ambaye alikuwa kumuona jana, amethibtisha na kusema kwamba ni kweli anatumia machine kwa kupumua, inatia huruma sana lakini hawana njia nyingine ya kufanya. Rais Zuma upande wake alijizuia kuzungumzia lolote kuhusu taarifa hii baada ya kupewa maelezo na ma daktari wanaomshughulikia rais Mandela wakati alipo tembelea Hospitalini jana saa nne usiku majira ya Afrika kusini, na Afrika ya kati, ikiwa ni saa tano usiku majira ya Afrika Mashariki.
Katika taarifa iliotolewa na rais Zuma, alifahamisha tu kwamba Nelson Mandela bado yupo katika hali ngumu na kutangaza kufuta ziara yake iliotarajiwa kufanyika mapema leo asubuhi nchini Msumbuji. Rais Zuma alipewa taarifa ya hali inayoendelea na madaktari wanaofanya kila jitihada kuhakikisha hali inaboreka zaidi.
Msemaji wake Mac Maharaj amezungumza kupitia kituo cha televisheni ya taifa hilo SABC kuwa kwa saa 48 zilizopita hali ya afya ya rais Mandela imekuwa mbaya zaidi, na hivo kusababisha rais Zuma kuahirisha safari yake nchini Msumbuji. Muda mchache kabla ya hapo Rais Zuma akiwa mbele ya watetezi wa vyama vya wafanyakazi alisema kuwa na matumaini ya kusherehekea miaka 95 ya Mandela Julai 18 huku akiomba watu kuendelea kumuweka yeye na familia yake katika mawazo yetu na sala za kila dakika. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO