Tuesday, June 25, 2013

JESHI LA LEBANON LAAPA KUWASAKA WASUASI WA KISUNNI

Jeshi nchini Lebanoni, limesema litaendelea na operesheni ya kuwasaka wafuasi wa kiongozi wa kidini dhehebu la Sunni mwenye msimamo mkali waliotekeleza mauaji ya wanajeshi 12 kusini mwa taifa hilo. Viongozi wa kijeshi wamethibitisha baada ya kikao cha dharura kilichofanyika mapema leo asubuhi na kuwashirikisha maafisa wote wa Usalama. Katika taarifa iliotolewa baada ya kikao cha dharura cha maafisa wa kijeshi na usalama, wameamuwa kuwasaka waasi na kuwasambaratisha hadi kwenye ngome yao ya cheikh Ahmad al Assir na kuwatia nguvuni wale wote walioleta choko choko kwa jeshi.
Kikao hicho cha dharura kiliongozwa na rais wa taifa hilo Michel Sleimane na kiliitishwa ili kutathimini muendelezo wa uperesheni ya kijeshi dhidi ya waasi waliohusika na mauaji ya wanajeshi 12 katika shambulio lililotokea jana katika mji wa Abra katika kitongoji cha mji wa bandari wa Saida.Katika taarifa iliotolewa na jeshi imewataka waasi walioshambulia wanajeshi na raia, kujisalimisha ili kuepusha umwagaji wa damu, na kwamba jeshi litaendelea na operesheni ya kuwafyeka wanaomiliki silaha katika mji wa Saida hadi pale usalama utaimarika.
Wakati huo huo vyombo vya sheria nchini humo vimemfungulia mashtaka Cheikh Al Assir na wafuasi wake 123.Mapambano yalianza jana Jumapili baada ya shambulio dhidi ya kituo cha wanajeshi ambapo wafuasi wa Cheikh Assir mwenye msimamo mkali wa kidini anaepingana na kundi la Hezbollah kundi la Kishia linalo pambano bega kwa bega kuusaidia utawala wa rais Bashar Al Assad.Kiongozi huyo wa kidini amejipatina umaarufu baada ya  msimao wake wa kuikosoa ya serikali ya Damascus na vikosi vya Hezbollah.
Hivi karibuni alilituhumu jeshi nchini humo kusalia kimya dhidi ya kundi la uasi lenye nguvu nchini humo la Hezbollah.Serikali ya Lebanoni, inaendelea na msimamo wake wa kutoegemea upande wowote katika mzozo wa Syria licha ya tuhuma ambazo zimeanza kutolewa tangu pale wapiganaji wa kundi la Hezbollah walipojiunga na majeshi ya Syria kuusaidia utawala wa rais Assad dhidi ya waasi ambao kwa asilimia kubwa ni wasuni, jambo ambalo laonekana kuzua mvutano kwa saaa nchini Liban

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO