Tuesday, June 25, 2013

RAIS WA UFARANSA AWASILI QATAR KUIJADILI SYRIA

Raisi wa Ufaransa Francois Hollande amewasili nchini Qatar tayari kwa mazungumzo juu ya mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yanayoendelea nchini Syria na kujadili mahusiano ya kiuchumi na taifa hilo lenye utajiri wa gesi.Raisi Hollande amejumuika nchini humo kufuatia mkutano wa mataifa rafiki za Syria katika siku iliyoamuliwa kutolewa haraka kwa msaada wa kijeshi kuwasaidia waasi wa Syria.
Aidha raisi Hollande alizungumza katika mkutano wake na wafaransa waishio Qatar na kusema kuwa amekaribisha maamuzi ambayo yataruhusu kuunga mkono upinzani nchini Syria ili kufikiwa lengo la kupatikana suluhu ya kisiasa.
Mawaziri kutoka uingereza, misri, ufaransa, Ujerumani, Italia, Jordan, Qatar, Saudi Arabia, Uturuki na marekani kwa pamoja walihudhuria mazungumzo hayo. Tamko la mwisho lilikuwa ni kwa kila nchi kwa namna yake ingetoa haraka mahitaji na vifaa vyote muhimu ili kuwawezesha waasi kuwalinda watu wa Syria pia kukabiliana na mashambulizi ya kikatili yanayofanywa na majeshi ya serikali na washirika wake.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO