Saturday, June 29, 2013

MAREKANI YAWAONYA RAIA WAKE WALIO MISRI

Serikali ya Marekani imetoa tahadhari kwa raia wake kutosafiri nchini Misri huku ikiwataka maafisa ambao hawajaajiriwa katika ubalozi wake nchini humo kuondoka mara moja kutokana na ghasia zinazoendelea . Baadhi ya raia wamefariki huku wengine wengi wakijeruhiwa vibaya kufuatia makabiliano kati ya wafuasi wa rais Mohammed Morsi na wale wa upinzani wakati ambapo rais huyo anatarajiwa kuadhimisha mwaka mmoja tangu achukue hatamu.
Maafisa nchini Misri wanasema kuwa kati ya waliouawa ni raia wa marekani mjini Alexandria. Tayari wananchi wa taifa hilo wameanza kununua chakula na mafuta kwa wingi ili kukihifadhi kwa hofu kwamba ghasia hizo huenda zikaenea. Wapinzani wa rais Morsi wanadai kuwa ameshindwa kutatua maswala nyeti nchini humo huku wafuasi wake wakisisitiza kuwa ni sharti apewe mda.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO