Wednesday, June 26, 2013

OFISI ZA CHAMA CHA MOSRI ZACHOMWA MOTO

Waandamanai wanaopinga serikali ya Rais Mohammad Morsi wa Misri wamechoma moto ofisi za chama chake cha Uhuru na Uadilifu ambacho ni tawi la kisiasa la harakati ya Ikhwanul Muslimin. Shirika la habari la al-Yaum Sub’h limeripoti kuwa, ofisi hiyo ilivamiwa na kuharibiwa kabla ya kuteketezwa katika mji wa Ibrahimia kaskazini mashariki mwa nchi. Habari zaidi zinasema kuwa, maafisa waandamizi wa chama hicho waliokuwa ofisini wakati wa tukio hilo walilazimika kukimbilia usalama wao katika msikiti uliokuwa karibu. Mali ya thamani kubwa imeharibiwa kwenye tukio hilo. Rais Morsi anakabiliwa na mashinikizo makubwa kutoka kwa wapinzani ambao wanadai uongozi wake wa mwaka mmoja haujaweza kutatua matatizo yanayowakabili Wamisri wa kipato cha chini. Wapinzani hao wakingozwa na shakhsia mashuhuri kama vile Mohammad el-Baradei na Amr Musa wamepanga kufanya maandamano makubwa Juni 30 ili kushinikiza kujiuzuu rais huyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO