Wednesday, June 26, 2013

WANAJESHI LIBYA WAULIWA NA WATU WENYE SILAHA

Wanajeshi wa Libya wasiopungua sita wameuawa baada ya watu wenye silaha wasiojulikana kukishambulia kituo cha upekuzi cha jeshi la nchi hiyo karibu na mji wa Sirte. Jeshi la Libya limeeleza kuwa askari jeshi hao wameuawa wakati watu kadhaa waliokuwa wamejizatiti kwa silaha walipokivamia kituo cha upekuzi cha kijeshi katika mji wa Sirte hapo jana. Jeshi la Libya limelizingira eneo hilo baada ya tukio hilo na tayari limeanzisha uchunguzi kuhusu shambulio hilo. Katika upande mwingine, wakazi wa mji wa Benghazi wameendelea kulalamikia kuzidi kuzorota hali ya usalama nchini Libya. Hadi kufikia sasa hakuna kundi wala mtu aliyekiri kuhusika nan shambulizi hilo la jana. Benghazi ambao ni mji wa pili kwa ukubwa nchini wa Libya katika wiki za hivi karibuni umeshuhudia wimbi la machafuko huku vituo kadhaa vya polisi vikiripuliwa kwa mabomu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO