Tuesday, June 25, 2013

WAPINZANI WA MURSI WAPANGA MAANDAMANO YA KUMNG'OA

Kiongozi mmoja nchini Misri Mahmoud Badr muasisi wa kampeni za kutaka kumg'oa rais Misri madarakani amesema Wananchi wa Misri wameoneka kugawanyika katika makundi mawili, yale ya wafuasi wa chama tawala cha Muslim bradhardhood pamoja na wale wa upinzani wanaomtaka rais Mohamed Morsi kuondoka madarakani, hali ambayo wachambuzi wa siasa wanaona kuwa inatishia kuzuka kwa machafuko nchini humo. Harakati zinaendelea nchini humo ambapo kapmeni ya Tamarod, ikimaanisha Uasi kwa kiarabu na tayari sahihi elfu kumi na tano zimekusanywa kuhakikisha wanapata idadi inayokubaliwa na sheria ili kuitisha uchaguzi mwingine kabla ya wakati.
Vyama kadhaa vya upinzani nchini humo vimejiunga na harakati za kuandamana kwa wingi mbele ya ikulu ya taifa hili Juni 30, ikiw ani tarehe ya kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuchaguliwa kwa rais Mohamed Morsi hali tete ya uchumi wa taifa hilo, uhaba wa mafuta, kukatika kwa umeme na kupandishwa kwa bei ya bidhaa mbalimbali nchini humo ndio imekuwa sababu ya kuwakusanya pamoja wananchi wa Misri chini ya kauli mbiu, kuuangusha utawala wa Muslim Bradherhood unaotuhumiwa kutaka kimabavu.
Hata hivyo swala hili limewagawa wananchi wa Misri ambao baadhi wanaumuunga Mkono rais na ambao wanahofia kuzuka kwa machafuko.Mohammed Hamed mkuu wa zamani wa baraza la kitaifa amesema kukusanya sahihi juu ya kumpinga raia au la haina athari yoyote kisheria, hili ni shinikizo la kisiasa.Mahmoud Badr yeye anasema kuwa kuanzisha kampeni Tamarod ni baada ya kuona kwamba rais Morsi ameshindwa, kisiasa, kiuchumi, kijamii na ameshindwa kutekeleza malengo ya mapinduzi ya mwanzoni mwa mwaka 2011 yaliompindua rais Hosni Moubarak.
Jumalililopita wafuasi wa chama tawala walijitokeza kwa wingi katika barabara za jijini Cairo kumuunga mkono rais Morsi huku wakidai kuwa rais haondolewi madarakani kwa maandamano. hii ni baada ya upinzani kuitisha maandamano makubwa Juni 30 wakati wa sherehe za kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuchaguliwa kwa rais Morsi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO