Tuesday, June 25, 2013

SERIKALI YA MALI YALALAMIKA KUBAKIA WANAJESHI WA UFARANSA

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Mali amekosoa vikali hatua ya Ufaransa ya kuendelea kuweko kijeshi katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.  Tieman Hubert Coulibaly amesema bayana kwamba, Mali haiwezi tena kuvumilia kuweko kwa wanajeshi takribani elfu moja katika ardhi ya nchi hiyo. Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Mali amesisitiza kwamba, Bamako haioni udharura wa kuendelea kuweko nchini humo majeshi ya Ufaransa ambayo yako katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo ya Kiafrika. Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Mali amesema, kuondoka majeshi ya Ufaransa nchini humo kutafungua haraka njia ya kupatikana amani katika ardhi ya nchi hiyo. Hayo yanajiri katika hali ambayo, hivi karibuni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon alikaribisha makubaliano ya amani yaliyotiwa saini kati ya serikali ya Mali na waasi wa Tuareg. Ban alisema katika ujumbe wake kwamba, pande mbili hizo zinafaa kuhakikisha kwamba makubaliano hayo yanatekelezwa kikamilifu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO