Tuesday, June 25, 2013

WAZIRI MKUU MISRI ATAHADHARISHA VITA YA KIMADHEHEBU

Waziri  mkuu  wa  Misri  ameshutumu  mauaji ya  Waislamu wanne  wa  madhehebu  ya  Shia  yaliyofanywa  na  kundi la  Wasunni  ambalo  linajumuisha  Wasalafi  wenye msimamo  mkali  katika  kijiji  karibu  na  mji  mkuu  Cairo. Taarifa  iliyotolewa  na  ofisi  ya  waziri  mkuu  Hesham Kandil leo imesema  kuwa  anafuatilia  kwa  karibu uchunguzi  kuhusu  tukio  hilo ili  kuhakikisha  kuwa wahusika  wanaadhibiwa.
Misri  ni  nchi  yenye  waumini  wengi  wa  madhehebbu  ya Sunni  ikiwa  na  idadi  ndogo  ya  Washia. Kiasi  ya asilimia  10  ya  wakaazi milioni  90  wa  nchi  hiyo  ni Wakristo. Shambulio  hilo  lililotokea  jana  Jumapili limekuja  wiki  moja  baada  ya  viongozi  kadha  wa  kundi la  Salafi  kuwakashifu  Washia  wakati  wa  mkutano uliohudhuriwa  na  rais  wa  nchi  hiyo Mohammed Mursi. Mmoja  wa  viongozi  hao  wa  kidini  Mohammed Hassan , amemtaka  Mursi  kutofungua  mpango  wa  Misri  kwa washia, akisema  kuwa  hawaingii mahali  bila  ya  kuleta ufisadi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO