Thursday, June 27, 2013

WABRAZIL WAZIDISHA MAANDAMANO YAO LICHA YA KAULI YA RAIS WAO

Waandamanaji nchini Brazil wameendelea na maandamano yao licha ya Rais wa taifa hilo, Dilma Rousseff kuahidi kufanya mabadiliko ili kuhakikisha anatii kiu ya wananchi wake kipindi hiki watu tisa wakitajwa kupoteza maisha kutokana na ghazi zinazo fuatia maandamano hayo. Maandamano makubwa yanaendelea kushuhudiwa nchini Brazil ambapo wananchi wanapiga kelele kufuatia kupanda kwa gharama ya maisha. Mamia ya waandamanaji wamejitokeza kwenye mitaa ya Rio De Janeiro na Sao Paoul na kufunga barabara wakionesha kuchukizwa na ahadi ambazo zimetolewa na Rais Rousseff ya kuhakikisha anaboresha huduma za usafiri, elimu na afya.
Jeshi la Polisi limelazimika kutumia nguvu kukabiliana na waandamanaji hao ambao wamesema hawapo tayari kuona fedha za umma zinatumika kwenye masuala ambayo hayana mchango kwenye maendeleo yao. Ghasia hizo zinaendelea kupindi hiki Rais Rousseff akiomba msaada kutoka katika Bunge kuhakikisha mabadiliko aliyoyatangaza yanaweza kufikiwa na hatimaye wananchi waweze kunufaika kupitia kodi zao. Waandamanaji hao wameweka bayana kabisa lengo lao ni kuzuia hata kufanyika kwa Kombe la Dunia lililopangwa kufanyika mwakani wakitaka fedha zinazotumiwa kwenye maandalizi hayo zitumike kuboresha maisha yao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO