Thursday, June 27, 2013

POLISI BRAZIL WAENDELEA KUKABILIANA NA MAANDAMANO

Jeshi la Polisi nchini Brazil linaendelea kukabiliwa na kibarua kigumu cha kupambana na waandamanaji ambao wameanza kutumia mbinu tofauti ikiwa ni pamoja na kufanya maandamano kwenye Kiwanja cha mpira kilichotumika kwa mchezo wa Nusu Fainali ya Kombe la Mabara. Ghasia kubwa zilizuka nje ya uwanja wa mpira wa miguu wa Belo Horizonte kutokana na waandamanaji kuanza kufanya fujo ikiwa ni sehemu ya shinikizo laokwa serikali iweze kusikiliza kilio chao cha kuboresha maisha ya wananchi.
Waandamanaji wapatao elfu arobaini wamejitokeza kwenye mitaa iliyokaribu na Uwanja wa Mpira wa Belo Horizonte na hivyo Jeshi la Polisi likalazimika kutumia mabomu ya machozi na risasi za mpira kuwasambaratisha watu hao. Takwimu zinaonesha watu milioni moja na laki mbili walijitokeza kwenye maandamano ya nchi nzima wakiendelea kushinikiza serikali ichukue hatua dhidi ya viongozi wala rushwa sanjari na kuboresha huduma za kijamii.
Maandamano hayo haya ya kulenga viwanja yanakuja kipindi hiki Rais Dilma Rousseff akitaka msaada kutoka kwa Bunge na Baraza la Seneti ili aweze kuharakisha mkakati wa kufanya mabadiliko yatakayosaidia kuboresha sekta za afya, elimu na usafiri.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO