Wednesday, July 24, 2013

ARBOUR ASEMA ICC IMEPOTEZA MWELEKEO WAKE

Mkurugenzi Mtendaji wa kundi la kimataifa la migogoro amesema kuwa, Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ilifanya makosa kutoa tuhuma  za kutenda  jinai za kivita na kibinadamu dhidi ya Rais Omar Hassan al Bashir wa Sudan. Louise Arbour ambaye alishawahi kuwa Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa na mjumbe wa kamati ya kimataifa ya uchunguzi huko Darfur magharibi mwa Sudan amesema kuwa, tuhuma zilizotolewa dhidi ya Rais al Bashir zimeidhoofisha nafasi ya mahakama ya ICC. Mahakama hiyo yenye makao yake The Hague nchini Uholanzi inamtuhumu Rais al Bashir kwa kutenda jinai za kivita na kibinadamu na imezitaka nchi za Kiafrika kumtia mbaroni  kiongozi huyo pindi atakapozitembelea nchi hizo. Hata hivyo, kikao cha wakuu wa Umoja wa Afrika kilichofanyika mwaka 2009 huko Sirte nchini Libya, kilichukua uamuzi wa pamoja wa kutoshirikiana na mahakama kuhusiana na mpango wa kumtia mbaroni Rais wa Sudan.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO