Wednesday, July 24, 2013

KIONGOZI MWANDAMIZI WA HAMAS APINGA MAZUNGUMZO NA ISRAEL

Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS ameukosoa vikali uamuzi wa Serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina wa kukubali kufanya mazungumzo ya mapatano na utawala haramu wa Israel na kusema hatua hiyo ni  sawa na kujiua kisiasa. Usama Hamdan amesisitiza kwamba, kufanya mazungumzo ya mapatano na utawala wa Kizayuni wa Israel hakuna natija yoyote ghairi ya kupoteza haki za Wapalestina na kimsingi ni kutoa pigo kwa kadhia nzima ya Palestina. Kiongozi huyo mwandamizi wa Hamas amemkosoa vikali Rais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina na kubainisha kwamba, daima Mahmoud Abbas amekuwa akisema kuwa, anafungamana na misingi thabiti ya Wapalestina, lakini katika vitendo hafungamani na misingi hiyo. Usama Hamdan ameongeza kuwa, kushiriki katika mazungumzo ya mapatano ya Washington sio tu kwamba, ni ujinga wa kisiasa bali ni kujiua kisiasa na kupoteza haki za wazi za Wapalestina. Amesema, kufanyika mazungumzo kama hayo hakuna wakati ambao yatazuia kuendelea jinai za Wazayuni dhidi ya Wapalestina sambamba na kuvunjiwa heshima matukufu yao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO