Saturday, July 20, 2013

HIZBULLAH YAITAKA ISRAEL KUANGALIA MIJI YAKE KABLA YA KUISHAMBULIA LEBANON

Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel  katika vita vijavyo  kwanza unapaswa  kufikia hatima ya miji ya utawala huo ghasibu  kabla ya kuishambulia Bairut, na kusisitiza kwamba Israel haina ubavu tena wa kuikalia kwa mabavu ardhi ya Lebanon. Sayyid Hassan Nasrullah amesisitiza kuwa, muqawama nchini Lebanon una mitazamo, malengo, majukumu, mikakati  na sera zilizokuwa wazi kabisa. Katibu Mkuu wa Hizbullah amesisitiza kuwa, utawala wa Israel na nchi zote zilizokuwa nyuma ya utawala huo ghasibu zinaelewa kwamba, si rahisi tena kuishambulia  kijeshi  Lebanon. Sayyid Hassan Nasrullah ameelezea sababu ya kuwa dhaifu jeshi la Lebanon na kusisitiza kuwa, Iran ilitangaza kuwa tayari kulijenga na kuliimarisha jeshi la Lebanon, lakini Marekani na baadhi ya nchi za Kiarabu zilipinga vikali kwa kuhofia kwamba jeshi la Lebanon litakuwa na nguvu zaidi katika eneo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO