Saturday, July 20, 2013

LIBYA YAONYA MAKUNDI YA WABEBA SILAHA

Wizara ya Mambo ya Ndani nchini Libya, imeyaonya makundi ya wabeba silaha yanayojihusisha na vitendo vya utekaji nyara nchini humo. Katika taarifa yake iliyoitoa leo, wizara hiyo imeyaonya makundi hayo yanayokwamisha mwenendo wa kisiasa nchini humo na kujihusisha na utekaji nyara wa binaadamu na kuahidi kuwachukulia hatua kali wahusika wa vitendo hivyo. Aidha wizara hiyo imeashiria ongezeko la vitendo hivyo na kusema kuwa, kumekuwepo vitendo vya utekaji nyara huku ikiahidi kuwepo mikakati madhubuti inayoandaliwa kwa minajili ya kukabiliana na hali hiyo. Imesisitiza kuwa, vitendo vya utekaji nyara, vinapingana na uhuru wa binaadamu, na kuwataka wananchi kushirikiana na serikali ili kuwatia mbaroni wahusika. Hii ni katika hali ambayo, katika wiki kadhaa za hivi karibuni, mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli, umekuwa ukishuhudia vitendo vya utekaji nyara na mateso ambavyo hufanywa na watu wenye silaha ambao walipewa ruhusa na wizara hiyo ya mambo ya ndani, kwa ajili ya kuimarisha usalama nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO