Wednesday, July 24, 2013

M23 WADAI KUWAUWA WANAJESHI 400 WA KONGO

Waasi wa M23 waliojizatiti katika eneo  la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamedai kuwauwa zaidi ya wanajeshi 400 wa serikali ya Kongo  mashariki mwa nchi. Taarifa iliyotolewa leo na waasi hao imeeleza kuwa, tokea yalipoanza mapigano mapya yapata siku 10 zilizopita karibu na mji wa Goma, makao ya jimbo la Kivu Kaskazini, zaidi ya wanajeshi 400 wa serikali ya Kongo wameshauawa na mamia ya wengine kujeruhiwa kwenye mapigano hayo. Luteni Kanali Vianney Kazarama Msemaji wa waasi wa M23 amesema leo kuwa, wanajeshi hao wa serikali wameuawa katika meneo ya Kibati na Kanyarucinya yaliyoko umbali wa kilomita 15 kutoka mji wa Goma. Wakati  huohuo, raia wasiopungua 10 wamejeruhiwa baada ya helikopta ya jeshi la Kongo kuwashambulia raia kimakosa  mashariki mwa nchi hiyo. Duru za hospitali zinasema kuwa, hali za baadhi ya majeruhi zimeripotiwa kuwa mahututi. Jeshi la Kongo limesema kuwa, shambulio hilo lililenga lilikusudiwa kulenga  ngome ya waasi wa M23 katika eneo la Rumangabo mashariki mwa nchi hiyo. Taarifa hiyo imeeleza kuwa, rubani alifanya makosa kwa kuwalenga  raia badala ya waasi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO