Sunday, July 28, 2013

MAANDAMANO MAKUBWA YAFANYIKA UJERUMANI

Maelfu ya watu wameandamana nchini Ujerumani kupinga mpango wa udukuzi wa Marekani. Waandamanaji hao wameitikia wito wa kundi linalojiita stopwatching us na kuvumilia joto na jua kali kuandamana katika miji ya Hamburg,Munich,Berlin na miji mingine 35 nchini humu.Baadhi ya waandamanaji hao walivaa kofia kubwa kuzuia jua huku wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe wa kutaka kukomeshwa kufuatiliwa kwa data za simu na mitandao.Huku hayo yakijiri,raia wengi nchini humu wamemiminika katika vidimbwi vya maji,maziwani na fuoni kupunguza makali ya joto ambalo limekuwa likiongezeka katika msimu huu wa kiangazi na kufikia nyuzi 39 za celisius.Wataalam wa utabiri wa hali ya hewa wamesema Ujerumani huenda  itarekodi kiwango cha juu zaidi cha nyuzi 40.2 hapo kesho ambacho mara ya mwisho kilishuhudiwa mwaka 1983.Mvua ya ngurumo wikendi hii inatarajiwa kuleta afueni kwa kiasi fulani kabla ya viwango vya joto kupanda tena wiki ijayo.   

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO