Friday, July 26, 2013

MAHAKAMA ISRAEL YARUHUSU KUTUMIWA SILAHA ZA KEMIKALI

Waziri wa Afya wa serikali iliyochaguliwa na wananchi wa Palestina inayoongozwa na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas amelaani vikali hatua ya Mahakama Kuu ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuruhusu utumiwaji gesi ya kemikali yenye mada za fosforasi nyeupe. Mufid al Mukhlalati amesema kuwa, hatua ya mahakama hiyo kuruhusu utumiwaji wa gesi hizo za kemikali zenye mada za fosforasi nyeupe, kunalipa nguvu jeshi la utawala huu kutengeneza silaha hatari za kemikali zitakazotumiwa dhidi ya wananchi wa Palestina. Tarehe 9 Julai mwaka huu, Mahakama Kuu ya Israel ilitangaza kuwa, utumiwaji wa gesi hiyo ya kemikali ni ruhusa kabisa. Waziri wa Afya wa Palestina amesema kuwa, hivi sasa mashirika ya kutetea haki za binadamu duniani yanafanya juhudi za kuzuia jinai zinazofanyika ulimwenguni kote, lakini vyombo vya sheria vya utawala wa Israel vinapuuzia sheria za kimataifa kwa kuruhusu utumiwaji wa gesi za kemikali zenye mada za fosforasi nyeupe.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO