Sunday, July 28, 2013

RAIS WA UJERUMANI ASEMA SNOWDERN ANASTAHILI HESHIMA

Rais wa Ujerumani Joachim Gauck ametoa ujumbe wa kumuunga mkono Edward Snowden, mfanyakazi wa zamani wa shirika la ujasusi la Marekani CIA aliyefichua siri za ujasusi unaofanywa na shirika hilo kuwa ni mtu anayestahili heshima kwa kutetea uhuru wa faragha wa mtu binafsi. Gauck ametoa kauli hiyo katika mahojiano aliyofanyiwa na gazeti moja la Ujerumani. “Mtu yeyote anayetoa taarifa kwa umma na kuchukua hatua kutokana na dhamiri ya nafsi yake anastahili heshima”, amesema Rais huyo wa Ujerumani. Ameongeza kuwa tangu mwezi uliopita wa Juni wakati Snowden alipofichua taarifa za shughuli za ujasusi unaofanywa na Marekani, binafsi amekuwa na mashaka makubwa na wasiwasi wa kuchelea kama kuna usalama kwa yeye kutuma barua pepe na kuzungumza kwa uwazi kabisa kwa kutumia njia ya simu. Rais wa Ujerumani ameongeza kama ninavyomnukuu: “hofu ya kuchelea kunaswa na kuhifadhiwa na mashirika ya kigeni ya ujasusi mazungumzo yetu ya simu au barua pepe yanabana hisia zetu za kujihisi kuwa tuko huru na wenye faragha”. Rais wa Ujerumani ameitaka serikali ya Kansela wa nchi hiyo Angela Merkel ifikie makubaliano na waitifaki wake yatakayoheshimiwa ya kudhamini uhuru wa faragha wa watu. Edward Snowden alifichua kuwa mashirika ya ujasusi ya Marekani hufanya udukuzi kote duniani kwa kutumia mbinu ya kiteknolojia ya siri kuchunguza mawasiliano ya simu ya watu, barua pepe na mawasiliano mengine

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO