Saturday, July 20, 2013

NIGERIA KUTUMA WANAJESHI DARFUR

Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa litatuma wanajeshi 800 katika jimbo la Darfur magharibi mwa Sudan ili kuisaidia serikali ya Khartoum na kikosi cha walinda amani wa Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa jimboni humo. Akiwahutubu wanajeshi hao watakaopelekwa huko Darfur, Ahmad Jibrin kamanda wa kikosi cha pili cha jeshi la Nigeria amevitaka vikosi hivyo kuheshimu haki za binadamu na utamaduni wa watu wa Sudan katika muda wote wakataokuweko huko Darfur wakilinda amani. Kamanda huyo wa jeshi la Nigeria amesema kuwa askari wake yoyote atakayetekeleza jinai au uhalifu jimboni Darfur atakabiliwa na hatua kali. Hii ni katika hali ambayo jeshi la Nigeria jana lilitangaza kuwa lina mpango wa kuondoa baadhi ya wanajeshi wake walioko kaskazini mwa Mali baada ya kuboreka hali ya mambo katika eneo hilo na baadaye kuwapeleka wengine.  

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO