Saturday, July 20, 2013

BUNGE LA IRAN KUICHUNGUZA BARUA KUHUSIANA NA MAREKANI

Bunge la Iran lapanga  kuchunguza barua ya wajumbe wa bunge la Congress ya Marekani ambayo walimuandikia Rais Barack Obama barua wakitaka afanye mazungumzo na rais-mteule wa Iran Dkt. Hassan Rohani.
Hayo yamedokezwa leo na Alaeddin Boroujerdi Mkuu wa Kamati ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni katika Majlis. Boroujerdi amesema kumekuwepo na ukosefu wa uthabiti katika maamuzi ya Congress kwani bunge hilo hivi karibuni  lilimtaka Obama aiwekee Iran vikwazo vipya na muda mfupi baadaye likamtaka rais huyo wa Marekani afanye mazungumzo na rais-mteule wa Iran.
Hivi karibuni zaidi ya wabunge 131 katika Baraza la Congress walisema kuchaguliwa Dkt. Rohani ni fursa ya kuleta maelewano baina ya Washington na Tehran na hivyo waliitaka Ikulu ya White House itumie njia za kidiplomasia katika kuamiliana na Iran.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO