Sunday, July 28, 2013

WAFUASI WA MORSI KUENDELEZA MAANDAMANO

Muungano unaoundwa na vyama vinavyoiunga mkono harakati ya Ikhwaanul Muslimiin nchini Misri umeahidi kuendeleza maandamano leo na kesho nchini humo. Taarifa zinasema kuwa, muungano huo umesisitiza kuendelezwa  maandamano ya kipinga hatua ya jeshi la nchi hiyo ya kumuondoa madarakani Rais Muhammad Morsi wa nchi hiyo. Waandamanji hao wataka Muhammad Morsi arejeshwe kwenye wadhifa wake wa rais wa nchi hiyo.
Hapo jana, mamilioni ya waungaji mkono wa Morsi walifanya maandamano kwenye miji mbalimbali nchini humo wakitangaza uungaji mkono wao kwa rais aliyechaguliwa kwa njia za kidemokrasia. Waandamanaji hao wanamtaka AbdulFattah as Sisi mkuu wa majeshi ya Misri ajiuzulu, kwa vile alitoa amri kinyume cha sheria ya kuenguliwa Morsi madarakani. Maandamano ya jana Ijumaa ya waungaji mkono na wapinzani wa Morsi yalisababisha watu watano kuuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa katika mji wa Alexandria.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO