Sunday, July 28, 2013

120 WAUAWA MISRI KATIKA MACHAFUKO

Watu wasiopungua 120 wameuawa na wengine zaidi ya 1500 kujeruhiwa katika mapigano yaliyojiri katika miji mbalimbali kati ya wafuasi na wapinzani wa Muhammad Morsi rais wa Misri aliyepinduliwa na jeshi la nchi hiyo.Mapigano hayo yalizuka jana baada ya wafuasi wa Morsi waliokuwa wamekusanyika katika wilaya ya al Nasr huko Cairo kudai kurejeshwa madarakani rais huyo. Aidha maandamano mengine yalifanyika hiyo jana kufuatia wito uliotolewa na harakati ya Ikhwanul Muslimin ya kufanya maandamano ya amani kupinga mapinduzi ya kijeshi yaliyomng'oa madarakani Rais Muhammad Morsi. Wakati huo huo habari zimeeleza kuwa  jeshi la Misri limekuwa likitumia silaha hai kwa wafanya maandamano   nchini humo. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO