Thursday, July 25, 2013

WALIOTOROKA JELA IRAQ KWENDA SYRIA

Kundi la kigaidi la al-Qaida la nchini Iraq limetangaza kuhusika na hujuma dhidi ya magereza ya Abu Ghureib na Taji ambapo zaidi ya wafungwa 500 walitoroka. Taarifa ya al-Qaeda imesema wafungwa hao wako tayari kupigana na serikali ya Rais Bashar Asad wa Syria na kwamba mipango inafanywa ili waelekee nchini humo. Katika hujuma hiyo kwenye magereza hayo mawili makubwa nchini Iraq, zaidi ya watu 50 waliuawa wakiwemo maafisa wa gereza huku wengine wengi wakijeruhiwa. Waziri Mkuu wa Iraq, Nouri al-Maliki amesema serikali yake itaendelea kukabiliana na magaidi na kwamba juhudi za kuwasaka wafungwa waliotoroka zinaendelea. Imebainika kwamba baadhi ya walinzi kwenye gereza la Abu Ghureib walishirikiana na magaidi kwenye hujuma hiyo iliyotokea Jumapili iliyopita.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO