Thursday, July 25, 2013

ZAMBIA YASEMA TOKA ULAYA INA KEMIKALI ZA SARATANI

Zambia imesitisha uagiziaji wa nyama ya ng'ombe kutoka bara Ulaya baada ya kubainika ina kemikali inayosababisha ugonjwa hatari wa saratani.BShirika kubwa zaidi la nyama ya ng'ombe Zambia, Zambeef, leo limetoa taarifa likisema, mada ya kemikali ijulikanayo kama aromatic aldehydes imepatikana katika nyama kutoka Ulaya hasa Uingereza.
Zambeef ilikusanya bidhaa zote za nyama ya ng'ombe katika maduka yake baada ya kubainika kuwepo kemikali hiyo ambayo pia hutumiwa kuhifadhi maiti. Mkurugenzi wa Zambeef Jacob Mwanza amesema kuanzia sasa shirika hilo litakuwa likinunua nyama ya ngo'ombe kutoka Zambia pekee. Katika miaka ya hivi karibuni nchi za Ulaya zimelaumiwa kuwa zinazitumia nchi za Afrika kama jalala la bidhaa ambazo zimepigwa marufuku barani humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO