Saturday, August 17, 2013

BARAZA LA USALAMA LATAKA KUJADILIWA MAUAJI YANAYOENDELEA MISRI

Baraza la usalama la umoja wa mataifa limefanya mkutano wa dharura kuzungumzia namna vikosi vya usalama vya Misri vilivyowaua wa Rais aliyeondolewa madarakani Mohamed Morsi na kusema kuna haja ya pande husika kuwa na "uvumilivu wa hali ya juu". Tamko hilo la baraza la usalma linakuja siku moja tu baada ya watu wapatao 638 kuuwawa wakati polisi walipokuwa wakiwatawanya waandamanaji wafuasi wa Muslim Bortherhood. Waandamaji hao wamekuwa wakitaka Bwana Morsi aliyeondolewa uongozini arudishwe maradaraki. Wakati huo huo rais wa Marekani Barack Obama ameshutumu hatua ya serikali ya muda ya Misri akisema haukuwa na sababu za kutosha.
"tunasikitishwa sana na unyama uliofanyiwa raia wa kawaida " , amesema Obama huku akitangaza kuwa zoezi la kijeshi la pamoja kati ya Marekani na Misri ambalo lilikuwa limepangwa kufanyika mwezi ujao umefutwa. Rais Obama amesema ushirikiano kati ya nchi hizo mbili hauwezi kuendelea wakati raia wanauwawa. Licha ya mauaji hayo na umwakikaji mkubwa wa damu ,lakini kikao hicho cha dharura cha umoja wa mataifa kilichoandaliwa mahusus kujadili swala la Misri kilikumbwa na mgawanyiko mkubwa baina ya wanachama 15 wa baraza hilo la Usalama. Wanachama hao 15 walishindwa kuafikiani kuhusu jinsi ya kukabiliana na hali ya Misri, huko jeshi likizidi kukaza kamba.
Kwa kawaida Urusi na China huwa zinapinga hatua yeyote ya baraza la usalama kuingilia maswala ya ndani ya nchi yeyote ile. Hivyo katika kikao hicho cha dharura , Urusi na China hazikibadili msimamo wao wa jadi , bado walipinga kuwa Misri na jeshi lisiingiliwe bali njia ya maridhiano itafutwe. Pengine hii ni kutokana na swala la Chechnya ambalo bado linaisumbua Urusi huko China ikihangaishwa na tatizo la Tibet. Taarifa zinasema China ilikataa katakata kutia saini taarifa rasmi ya baraza la usalama la kulishutumu jeshi la Misri kwa kusababisha umwagikaji wa damu na mauaji.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO