Saturday, August 17, 2013

LIBYA KUSHAMBULIA MELI ZA MAFUTA HARAMU

Waziri Mkuu wa Libya,Ali Zeidan ametishia kutumia nguvu kuwazuia walinzi katika bandari kuu nchini humo dhidi ya kuuza mafuta kwa mashirika ya kibinafsi.Afisa huyo amesema meli yeyote itakayotia nanga katika bandari za Libya bila idhini ya serikali itashambuliwa kwa bomu.Wafanyikazi wa badari wamekua kwenye mgomo wiki kadhaa sasa kulalamikia malipo. Maafisa wamesema mgomo huo umesababisha kupungua kwa mauzo ya mafuta nchini Libya na hivyo kuathiri vibaya uchumi wa nchi.
Waziri Mkuu amesema serikali itatumia nguvu zozote zile kuzuia kile amesema kuvuruga biashara ya mafuta. Banadari zilizoathirika na mgomo ni pamoja na Zeitunia, Brega, Ras Lanouf na Sedra. Uzalishaji wa mafuta Libya ulipungua hadi mapipa laki sita kutoka mapipa milioni moja baada ya kuzuka mapinduzi dhidi ya kiongozi wa zamani Kanali Muammar Gaddafi mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO