Thursday, August 15, 2013

KEITA ASHINDA DURU YA PILI YA UCHAGUZI MALI

Serikali ya Mali imetangaza kuwa, Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo, Ibrahim Boubacar Keita ameshinda duru ya pili ya uchaguzi wa rais kwa kujipatia asilimia 78 ya kura. Serikali pia imesema idadi jumla ya waliopiga kura ilipungua kutoka asilimia 49 kwenye duru ya kwanza hadi asilimia 46 kwenye duru ya pili. Keita alipata uungaji mkono kutoka kwa wagombea 22 kati ya 25 aliowashinda kwenye duru ya kwanza. Weledi wa mambo wanasema ushindi huo mnono aliopata Keita ni kibali rasmi kutoka kwa wananchi cha kufanya mazungumzo na waasi wa kaskazini ili kutatua mgogoro ulioko kwa njia ya amani. Keita anakabiliwa na changamoto chungu nzima lakini kubwa zaidi ni jinsi ya kulikarabati jeshi la nchi hiyo ambalo mwaka uliopita lilimpindua rais Amadou Toumane Toure. Waziri Mkuu huyo wa zamani amesema ataunda serikali yenye sura ya kitaifa itakayowaleta pamoja wananchi wote wa Mali.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO