Sunday, August 18, 2013

HOFU YA WAPALESTINA WALIOGOMA KULA

Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu limeelezea wasiwasi wake kuhusu hali ya wafungwa saba wa Kipalestina ambao wamesusia chakula katika jela za kuogofya za utawala wa Kizayuni wa Israel. Katika taarifa siku ya Jumamosi, shirika hilo lilisema kunapaswa kutafutwa suluhisho kuhusu wafungwa hao. ICRC imesema ina wasiwasi mkubwa hasa kuhusu mfungwa aitwaye Imad Abdelaziz Abdallah al-Batran ambaye amesusia chakula kwa wiki kadhaa sasa. Wafungwa hao Wapalestina wamesusia chakula kulalamikia hali mbaya katika jela hizo za utawala wa Israel.
Mapema mwezi huu Wizara ya Masuala ya Wafungwa Palestina ilisema utawala haramu wa Israel unawashikilia Wapalestina 5,100 wakiwemo watoto 250 na wanawake 14 katika gereza 17. Wakuu wa jela za kuogofya za Israel wamekuwa wakikiuka haki za binadamu za wafungwa wa Palesitna kama vile kuwashikilia pasina kuwafunguliwa mashtaka na kuwatesa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO