Sunday, August 18, 2013

ISRAEL YAOMBAMSAADA ZAIDI WA KIJESHI TOKA MAREKANI

Maafisa wa Marekani na wa utawala wa Kizayuni wa Israel wanajadili kuongeza kiwango cha fedha za msaada wa kijeshi wa Washington kwa Tel Aviv huku pande hizo mbili zikishauriana kuhusu msaada mpya wa kijeshi kwa kipindi cha miaka 10 ijayo. Jarida la Defense News limeripoti kuwa chini ya makubaliano ya sasa ya msaada huo uliosainiwa na pande mbili mwaka 2007, dola bilioni 30 za walipa kodi wa Marekani zinamiminwa kwenye mfuko wa hazina wa Israel. Hata hivyo Utawala wa Kizayuni umekuwa na wasiwasi kutokana na kuongezeka uuzaji silaha za Marekani kwa nchi za Mashariki ya Kati na hivyo unaitaka Washington kuuongezea kitita cha fedha katika msaada wa kuipatia silaha za kisasa zaidi. Msaada wa kila mwaka wa kijeshi unaotolewa na Marekani kwa Israel umeongezeka kutoka dola bilioni 2.4 hadi dola bilioni 3.1, ambapo kwa mujibu wa makubaliano ya sasa kiwango hicho kitaendelea hadi mwaka 2017. Wakati alipofanya safari huko Israel ambayo ni ardhi ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu mnamo mwezi Machi mwaka huu, Rais Barack Obama wa Marekani alisema ameafiki kuanza kufanya majadiliano na Israel juu ya kurefusha kipindi cha utoaji msaada wa kijeshi kwa utawala huo haramu

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO