Sunday, August 18, 2013

RAJOELINA NA LALAO WAZUIWA UCHAGUZI

Korti inayosimamia masuala ya uchaguzi nchini Madagascar imeyakataa maombi ya kugombea kiti cha rais,rais wa sasa Andry Rajoelina na Lalao Ravalomanana, ambae ni mke wa rais wa zamani.Taasisi hiyo imeyakataa pia maombi ya rais wa zamani Didier Ratsiraka.Korti ya uchaguzi imehalalisha uamuzi huo kwa kile ilichokiita "kasoro zilizojitokeza katika kufuatwa sheria" na korti ya awali ya uchaguzi.Uamuzi huo umelenga kutuliza hofu za jumuia ya kimataifa kuhusu kuitishwa uchaguzi huo.Umoja wa Afrika ulioshikilia wagombea wote watatu wasiruhusiwe kupigania kiti cha rais,pamoja pia na Ufaransa na jumuia ya maendeleo kusini mwa Afrika-SADC,umesema uamuzi huo wa korti ya uchaguzi ni hatua muhimu katika kupatikana masharti yanayohitajika kuitisha uchaguzi wa rais kwa njia za uwazi na kuaminika.
                    

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO