Sunday, August 18, 2013

WANAWAKE WA KIISLAM WAANDAMANA UFARANSA

Wanawake wa Kiislamu nchini Ufaransa wamefanya maandamano kutetea vazi la stara ya Kiislamu la Hijabu. Maandamano hayo yalifanyika jana katika eneo la Trappes huko kaskazini mwa nchi hiyo. Wanawake hao wa Kiislamu wameandamana kulalamikia ongezeko la mashambulio yanayotokana na chuki dhidi ya Uislamu wanayofanyiwa wanawake wanaovaa hijabu na kupinga ushadidishaji wa sheria zinazoweka mipaka ya uvaaji hijabu nchini Ufaransa. Maandamano hayo yalianzia mbele ya msikiti wa eneo la Trappes hadi kwenye jengo la Manispaa ya eneo hilo. Maandamano ya jana yamefanyika kufuatia mashambulio ya mara kwa mara dhidi ya wanawake wa Kiislamu wanaovaa hijabu na kushindwa polisi kukabiliana na vitendo hivyo katika mji huo wa Trappes. Mbali na Polisi ya Trappes kushindwa kukabiliana na mashambulio yanayofanywa dhidi ya wanawake wa Kiislamu wanaovaa hijabu, inatuhumiwa pia kushirikiana na watu wenye chuki na Uislamu katika kufanya vitendo vya kibaguzi na miamala miovu dhidi ya Waislamu

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO