Wednesday, August 07, 2013

JUHUDI ZA KIDIPLOMASIA ZAKWAMA MISRI

Juhudi za wanadiplomasia wa mataifa ya Magharibi na Uarabuni kumaliza msuguano wa kisiasa kati ya serikali ya mpito nchini Misri na wafuasi wa chama cha kiislam cha Muslim Brotherhood zimeshindwa, ofisi ya raisi imesema leo Jumatano. Taarifa hiyo inaona kuwa kwa sasa serikali inaweza kuanzisha harakati dhidi ya wafuasi wa rais aliyeondolewa madarakani Mohamed Morsi, hatua ambayo jumuiya ya kimataifa inahofu kuwa inaweza kusababisha umwagaji damu zaidi.
Maseneta wa Marekani John McCain na Lindsey Graham ambao wamekuwa nchini Misri kujaribu kutatua mzozo wa kisiasa nchini humo wamesema umwagaji damu huenda ukashuhudiwa nchini humo ikiwa suluhu la kudumu halitapatikana nchini humo na viongiozi wa Muslim Brotherhood wanaozuiliwa kuachiliwa huru. Duru zinasema kuwa wasuluhishi hao walishindwa kuafikiana na serikali ya mpito chini ya rais Adly Mansour ambaye amesema hatakubali mataifa ya kigeni kuingilia masuala yao.
Serikali ya mpito inaendelea kushikilia msimamo kuwa chama cha Muslim Brotherhood kinawajibika kwa kushindikana kwa juhudi hizi, na kwa ajili ya matukio yanayohusiana na ukiukwaji wa sheria na kuhatarisha usalama wa umma.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO