Wednesday, August 07, 2013

WAFANYAKAZI WA BALOZI ZA MAREKANI NA UONGEREZA WAONDOLEWA YEMEN

Marekani na Uingereza zimewaondoa wafanyikazi wake wa balozi zao kutoka mjini Sana'a nchini Yemen kufuatia hofu ya kufanywa kwa shambulizi la kigaidi.Hatari hiyo kubwa ya shambulizi linaloaminika kupangwa na mtandao wa kigaidi wa Al Qaeda pia imesababisha kufungwa kwa muda kwa balozi 19 mashariki ya kati na nchi kadhaa za Afrika.Hii inakuja baada ya Marekani wiki iliyopita kutoa tahadhari kote ulimwenguni kuhusu tisho la kigaidi.Ubalozi wa Ujerumani nchini Yemen pia umefungwa kwa muda kutokana na sababu hizo za kiusalama.Yemen imeimarisha usalama wake katika mitaa ya mji mkuu Sana'a.Wizara ya mambo ya ndani ya nchi hiyo imesema wanamgambo walikuwa wamepanga kushambulia ofisi na mashirika ya kigeni.Shambulio lililofanywa na ndege za Marekani zisizoendeshwa na marubani nchini Yemen hapo jana ziliwaua watu wanne wanaodaiwa kuwa wanachama wa Al Qaeda.Rais Obama amesema tisho hilo ni kubwa mno kiasi ya kuifanya Marekani kuchukua kila tahadhari.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO