Wednesday, August 07, 2013

MAWASILIANO YA VIONGOZI WA ALQAEDA NA MAREKANI KUFUNGWA


Imebanika kuwa mawasiliano kati ya viongozi wakuu wa Al Qeada akiwemo Ayman al-Zawahiri kiongozi wa kundi hilo yalisababisha Marekani kuamua kufunga balozi zake Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini kuanzia siku ya Jumapili iliyopita. Vyombo vya habari nchini Marekani vinaripoti kuwa shirika la Ujasusi nchini humo lilifanikiwa kunasa mawasiliano hayo kabla ya hatua kuchukuliwa.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani Jayne Carney amesema kuwa walichukuwa hatua hiyo kuwalimda raia wake dhgidi ya magaidi hao ambao wameendelea kuwasaka. Mbali na Mashariki na ya Kati na kaskazini mwa Afrika, Balozi za Marekani nchini Mauritiuys, Madagascar, Bunjumbura Burundi na Kigali Rwanda pia zimefungwa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO