Monday, August 12, 2013

KURA ZAANZA KUHESABIWA MALI

Zoezi la kuhesabu kura za uchaguzi wa duru ya pili ya uchaguzi wa Rais uliofanya hapo jana nchini Mali limeanza huku wananchi wa nchi hiyo wakiwa na matumaini kwamba, Rais ajaye ataleta uthabiti katika nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika. Mamilioni ya wananchi wa Mali jana walishiriki kwenye duru ya pili ya uchaguzi wa Rais baada ya duru ya kwanza kukosa kutoa mshindi. Waangalizi wa uchaguzi wa Mali wamesema kuwa, uchaguzi wa jana ulikuwa huru na wa haki. Matokeo ya mwisho ya uchaguzi wa Mali yanatarajiwa kutangazwa katika kipindi cha siku mbili au tatu tangu kufanyika uchaguzi huo na Mahakama ya Katiba ina muda wa hadi kufikia siku ya Ijumaa kuthibitisha matokeo hayo. Weledi wa mambo wanasema kuwa, Rais ajaye nchini Mali kati ya Ibrahim Keita au Soumaila Cisse, atakuwa na majukumu makubwa na mazito zaidi, hasa kwa kuzingatia mgogoro na matatizo chungu nzima yanayoikabili nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO