Friday, August 09, 2013

MARUBANI WA UTURUKI WATEJWA NYARA

Watu waliokuwa na  silaha leo wamewateka nyara marubani wawili wa ndege kutoka Uturuki,  kwenye njia ya uwanja wa ndege wa Beirut. Waziri wa  ndani wa Lebanon Marwan Charbel aliliambia Shirika la habari la AFP kwamba tukio hilo lilitokea mapema alfajiri wakati wahudumu wa shirika la ndege la Uturuki walipokuwa wakielekea uwanja wa ndege kutoka hoteli. Duru zinasema watu wanne waliokuwa na silaha walihusika. Waziri Charbel alisema amezungumza na  balozi wa Uturuki nchini Lebanon na kwamba uchunguzi umeanza, ikiwa ni pamoja na kumhoji dereva wa basi. Utekaji nyara huo unaaminiwa kuwa tukio linalohusiana na kutekwa nyara nchini Syria  kwa  Walebanon 9 wa madhebu ya shia  mwezi Mei mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO