Monday, August 12, 2013

W/MKUU WA PALESTINA ASEMA HAKUNA FAIDA MAZUNGUMZO NA ISRAEL

Waziri Mkuu wa serikali halali iliyochaguliwa na wananchi wa Palestina amesema kuwa, kuanza tena mazungumzo ya mapatano baina ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina na utawala wa Kizayuni wa Israel hakuna faida yoyote ile. Ismail Hania amesisitiza kuwa, mazungumzo hayo yatapelekea kuongezeka ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi katika maeneo ya Wapalestina. Waziri Mkuu wa serikali halali ya Palestina inayoongozwa na HAMAS amesisitizia udharura wa kutekelezwa maridhiano ya kitaifa ya Palestina na kuongeza kwamba, serikali ya Hamas inapinga kuweko mazungumzo hayo kwani hayana faida yoyote ile kwa Wapalestina. Hayo yanajiri katika hali ambayo, makundi ya mapambano ya Palestina yameendelea kusisitiza kwamba, kuanza mazungumzo eti ya mapatano yameufanya mwenendo wa utekelezaji makubaliano ya maridhiano ya kitaifa kuwa mgumu zaidi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO