Monday, August 19, 2013

MAANDAMANO YAFANYIKA YEMEN KULAANI MATUMIZI YA DRONE

Maelfu ya Wayemeni jana walimiminika kwenye mitaa ya Sana'a mji mkuu wa Yemen wakipinga kushtadi mashambulizi ya drone yaani ndege za Marekani zisizo na rubani nchini humo. Waandamanaji hao pia wamelaani mashambulizi ya hivi karibuni ya ndege za Marekani zisizo na rubani yaliyoua karibu watu 40 katika maeneo mbalimbali ya Yemen. Wananchi wa Yemen wanasema kuwa mashambulizi ya drone za Marekani yanawalenga wao katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo na kuitaka serikali ya Sana'a kutafuta suluhisho kwa mashambulizi hayo ya Marekani. Tarehe 16 mwezi huu pia raia wa Yemen walifanya maandamano huko Sana'a wakiilaumu serikali ya nchi hiyo wakisema kuwa inaunga mkono ajenda za kigeni na kupuuza matakwa ya wananchi. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO