Monday, August 19, 2013

WAZIRI MKUU WA MISRI ATAKA KUTOINGILIWA MASUALA YA NDANI YA NCHI HIYO

Serikali ya mpito ya Misri imezitaka baadhi ya nchi kuacha kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo. Nabil Fahmy Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri amesema kuwa Cairo inapinga uingiliaji wowote wa kigeni katika masuala yake ya ndani. Fahmy amesema matukio ya sasa huko Misri ni masuala ya ndani na kwamba uingiliaji wa nchi za nje utazidisha tu ghasia na machafuko nchini humo.  
Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri ameyasema hayo katika hali ambayo nchi nyingi duniani zimelaani jinai iliyofanywa na serikali ya mpito ya Misri kufuatia kuuliwa ovyo raia na jeshi la nchi hiyo wakiwemo wanawake. Nchi mbalimbali duniani zimetaka kusimamishwa mara moja mashambulizi ya jeshi la Misri dhidi ya raia. Mamia ya wafuasi wa Muhammad Mursi rais wa Misri aliyepinduliwa na jeshi la nchi hiyo wameuliwa na maelfu ya wengine kujeruhiwa katika mashambulizi yaliyofanywa na vikosi vya jeshi dhidi ya wafuasi hao.  

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO