Wednesday, August 07, 2013

MAELFU WAANDAMANA KUPINGA SERIKALI YA TUNISIA

Maelfu ya waandamanaji wamefanya maandamano katika mji mkuu wa Tunisia,Tunis, kutaka serikali inayoongozwa na wanasiasa wa kiisilamu kujiuzulu. Ni maandamano makubwa zaidi kutokea tangu mgogoro wa hivi karibuni wa kisiasa kuanza wiki mbili zilizopita kufuatia mauaji ya mwanasiasa mashuhuri Mapema baraza la kikatiba lilihirisha kazi yake hadi serikali na upinzani zitakapoanza mazungumzo. Baraza hilo linaandika katiba mpya ya nchi.
Maandamano hayo yaliitishwa na upinzani unaotaka baraza la kikatiba kuvunjiliwa mbali pamoja na serikali kujizulu na kuadhimisha miezi sita ya mauaji ya kiongozi mashuhuri wa upinzani Chokri Belaid. Chama cha kitaifa chenye ushawishi mkubwa nchini Tunisia ndicho kiliitisha maandamano ya wanachama wake laki sita kikiwataka kujiunga na maandamano ya wananchi. "watu wanataka utawala huu kuondolewa,'' walisema waandamanaji. Msemaji wa baraza la kikatiba, Mustapha Ben Jaafar, alisema kuwa kazi itaendelea kuhakikisha kuwa katiba mpya inaundwa pindi mazungumzo yatakapofanyika. Bwana Ben Jaafar, ambaye chama chake ni sehemu ya baraza la mawaziri, alikosoa wanasiasa kwa kukosa kuelewana ili kutatua mgogoro unaokumba taifa hilo.
Kumekuwa na maandamano karibu kila siku wananchi wakitoa wito wa kufutiliwa mbali kwa baraza la katiba tangu mwanasiasa huyo mashuhuri kuuawa. Mohamed Brahmi aliuawa tarehe 25 mwezi Julai , takriban miezi sita baada ya kuuawa kwa bwana Belaid, ambaye alikuwa mwanasiasa wa mrengo wa kushoto. Zaidi ya wanachama 70 wa baraza hilo walijiuzulu kwa upinzani kufuatia mauaji ya wanasiasa hao na kupanga maandamano ya kukesha nje ya makao makuu ya baraza hilo mjini Tunis.Punde baada ya katiba kuandikwa , uchaguzi mpya utafanyika mwezi Disemba. Mgogoro huu wa kisiasa ndio mbaya zaidi kushuhudiwa Tunisia tangu kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa rais Zine al-Abidine Ben Ali kufuatia mapinduzi ya kiraia Januari 2011.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO