Wednesday, August 07, 2013

MAWAZIRI WA MAMBO YA KIGENI NA USALAMA WA URUSI NA MAREKANI KUKUTANA

Mawaziri wa mambo ya kigeni na masuala ya ulinzi kutoka mataifa ya Marekani na Urusi wanatarajia kukutana Ijumaa hii huko Washington Marekani kufuatia mvutano unaozidi baada ya serikali ya Moscow kumpatia hifadhi mfanyakazi wa zamani wa shirika la kijasusi nchini Marekani, Edward Snowden. Maafisa nchini marekani wamearifu kuwa mkutano huo utawakutanisha waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry na wa masuala ya usalama Chuck Hagel, na wale wa Urusi Sergei Lavrov na Sergei Shoigu.
Taarifa ya Ikulu ya Marekani imesema kufuatia hoja ya Snowden Marekani inatathimini upya manufaa ya mkutano uliopangwa kuwakutanisha Rais wa marekani Barack Obama na wa Urusi Vladimir Putin mapema mwezi Septemba. Ikulu ya Marekani imebainisha pia miongoni mwa agenda zitakazojadiliwa katika mkutano wa viongozi hao kuwa ni hali ya mambo nchini Syria mpango wa kukomesha silaha za nyuklia,vilevile Afghanstan na Iran.


No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO