Monday, August 12, 2013

MZAZI WA SNOWDERN AMKOSOA OBAMA

Baba wa jasusi wa zamani wa Marekani, Edward Snowden amesema kuwa, Rais Barack Obama wa Marekani anaipotosha jamii ya nchi hiyo.
Lon Snowden ameyasema hayo katika mahojiano na shirika la habari la ABC na kusisitiza kuwa, matamshi ya Obama yaliyojengeka juu ya kuweka sheria za kuwalinda wafichua siri za nchi hiyo mfano wa Snowden, yako mbali na ukweli wa mambo, au yanapingana na washauri wake au yana lengo la kuipotosha jamii ya Wamarekani.
Siku ya Ijumaa iliyopita Rais Barack Obama wa Marekani aliwambia waandishi wa habari kuwa, kabla ya jasusi huyo kufichua siri, alikuwa amekwishatia saini muswada wa kuwalinda wafichuaji siri za nchi hiyo. Kwa upande mwingine Lon amevituhumu vyombo vya usalama na vya sheria vya Marekani akisema haviwezi kumhukumu kwa uadilifu mwanaye.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO