Monday, August 12, 2013

ISRAEL YASEMA HIZBULLAH WANAPATA UZOEFU TOKA SYRIA

Kamanda mmoja wa jeshi la utawala haramu wa Israel amesema kuwa, hatua ya harakati ya Hizbullah ya Lebanon kuingia katika mapambano na makundi ya kigaidi nchini Syria inawafanya wapiganaji wa harakati hiyo wajinoe zaidi kwa ajili ya kukabiliana na Israel.
Yaron Formosa amedai kuwa, hatua ya Hizbullah kuingia katika vita dhidi ya magaidi nchini Syria si kwamba itadhoofisha uwezo wa harakati hiyo, bali kutazidisha maradufu uzoefu wake katika kupambana na Israel. Yaron ameongeza kuwa, Hizbullah inafuatilia kwa karibu sana harakati zote za jeshi la utawala wa Israel katika mipaka ya Lebanon. Amezidi kuongeza kuwa, wapiganaji wa harakati hiyo, wamejipatia uzoefu mkubwa wa kutumia silaha za aina mbalimbali huko nchini Syria, suala ambalo linaitia wasiwasi mkubwa Israel.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO