Wednesday, December 26, 2012

MAMIA YA WATOTO KONGO WAMETENGANA NA WAZAZI WAO


Shirika la Kuwahudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (Unicef) limeripoti kuwa mamia kadhaa ya watoto wanaendelea kutengana na kuishi mbali na wazazi wao huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya karibu raia milioni moja kukimbia mapigano ya hivi karibuni huko mashariki mwa nchi hiyo. Unicef imetangaza kuwa jumla ya watoto 776 wakiwemo wa kike 429 walio na umri kati ya miezi sita na miaka kumi na nne wanalelewa na ndugu wa familia mwezi mmoja baada mapigano yaliyojiri kati ya vikosi vya serikali ya Kongo na waasi wa harakati ya M23 kwa ajili ya kuudhibiti mji muhimu wa Goma kuwalazimisha karibu watu milioni kuzikimbia nyumba zao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO