Monday, January 07, 2013

CHINA YAANZA UJENZI WA NISHATI YA NYUKLIA

Shirika  la  habari  la  China  limesema  kuwa  nchi  hiyo  imeanza ujenzi  wa  kinu  kipya  cha  kinuklia  kwa  ajili  ya  kujipatia  nishati, baada  ya  hatua  ya kuzuwia  ujenzi  kwa  muda  kufuatia maafa yaliyotokea Fukushima  nchini  Japan. Shirika  la  habari  la  Xinhua limesema  kuwa  kinu hicho  cha  nishati  kitakachogharimu euro milioni 365 katika  mji  wa  pwani  ulioko  mashariki  mwa  nchi  hiyo katika  jimbo  la   Shandong, kitakuwa  na vifaa  vya  usalama  vya hali  ya  juu  vilivyotengenezwa  na  watafiti  wa  China. China  ni nchi  inayotumia  nishati  nyingi  duniani  na  nishati  ya  kinuklia  ni muhimu  katika  juhudi  za  nchi  hiyo  kuzuwia  mahitaji yanayoongezeka  kwa  matumizi  ya vyanzo  vingine  kama  mafuta. China  ilisitisha  uidhinishaji  wa  vinu  vipya  vya  nishati  kufuatia tetemeko  la  ardhi  nchini  Japan  mwaka  2011  na  Tsunami iliyoharibu  mtambo  wa  kinuklia  wa  Fukushima. Hatua  hiyo  ya usitishaji  wa  ujenzi  iliondolewa  mwezi  Oktoba.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO