Tuesday, April 02, 2013

MISRI YAKATAA KUREJESHA BALOZI WAKE TEL AVIV


Msemaji wa Rais Muhammad Mursi wa Misri amekadhibisha vikali uvumi wa kurejeshwa balozi wa Misri huko Tel Aviv, Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
Ihab Fahmy amesema kuwa, hadi sasa hakuna mazungumzo yoyote yaliyofanyika juu kuanzishwa tena shughuli za kidiplomasia kati ya pande mbili. Mwezi mmoja uliopita, viongozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel waliwataka viongozi wa Misri wamrejeshe Atif Salim balozi wa nchi hiyo mjini Tel Aviv. Misri iliamua kumuita nyumbani Atif Salim, ikilalamikia hatua ya kichokozi na isiyo ya kibinadamu ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kushambulia eneo la Ukanda wa Gaza mwezi Novemba mwaka jana.
Duru za Israel pia zimeeleza kusikitishwa kutokana na kukosekana kiunganishi cha mawasiliano kati ya Rais Mursi na viongozi wa utawala wa Israel.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO